Monday, October 10, 2016

RAMOS NJ'E MWEZI MMOJA

Sergio Ramos akiugulia maumivu hapo jana baada ya kuumia
Baada ya hapo jana Hispania kukaribia kufuzu Kombe la Dunia kwa kuichapa 2-0 Albania ambayo ilionekana tishio kwa taifa hilo, hata hivyo ililazimika Ramos kutolewa sababu ya kuumia goti kwenye mchezo huo.
Na beki huyo atakuwa nj'e kwa mwezi mmoja kufuatia jeraha hilo ambalo lilifanya nahodha huyo kutolewa nj'e dakika ya 80 na David Silva kuchukua cheo hicho jana.  

Ramos ambaye alipumzishwa na  Los Blancos kwenye mechi ya ligi iliyopita hali ambayo itapelekea kuigharimu Madrid ambayo imepanga kutopoteza hata pointi moja baada ya kucheza michezo minne mfululizo bila ushindi, hivyo anatarajiwa kupona haraka ingawa kwa mwezi mmoja ni muda mrefu kwa mchezaji ambaye ni muhimu kwao.

No comments:

Post a Comment