Saturday, October 8, 2016

MWBEMBWE ZILIMPONZA NEYMAR.

Neyamar akitazamwa jeraha lake alilolipata kutoka kwa mchezaji wa Bolivia.
''Neymar anapaswa kuacha mbwembwe akiwa na mpira na kuheshimu maadui zake.'' Hiyo ni kauli ya mchezaji wa Bolivia Yusman Duk.
Duk aliyasema hayo baada ya kumpa jeraha la kichwani nyota huyo wa Brazil wakati wanagombania mpira kwenye mechi ambayo Brazil ilishinda 5-0. 
Duk na Neymar wakigombea mpira kwenye mechi hiyo.
Wakati akijaribu kumpiga chenga mshambuliaji wa New York Cosmas Yusman Duk, Neymar alionekana na jeraha kichwani hali iliyopelekea kutoka kwa damu nyingi eneo hilo la kichwa.   

''Soka ni mawasiliano katika michezo, nilijaribu kuchukua mpira na tayali nilishamsoma harakati zake za kutaka kuuchukua mpira nyuma yangu , basi na mimi nikampelekea mkono wangu kwake.'' Duk aliwaambia waandishi wa habari.

No comments:

Post a Comment