Tuesday, October 11, 2016

POGBA ATUPIA UFARANSA IKIIFUNGA UHOLANZI.

Paul Pogba akishangilia bao lake dhidi ya Uholanzi hapo jana.
Hapo jana Paul Pogba alikuwa shujaa kwa taifa lake la Ufaransa baada ya kuifungia bao kwenye mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Uholanzi jijini Amsterdam, mchezo ambao ulimalizika kwa 1-0.
Akipokea pasi kutoka kwa Dimitri Payet dakika ya 30 na kufanya kitu ambacho kila mtu alifurahishwa nacho kutoka kwa nyota huyo wa Manchester United. 

Ikiwa ni miezi michache ambapo mchezaji huyo alikuwa kwenye kitimoto juu ya kiwango chake baada ya kumalizika kwa michuano ya Euro 2016 ambapo Ufaransa walipoteza fainali kwa Ureno. 
 

No comments:

Post a Comment