Saturday, September 24, 2016

ARSENAL HAWATAKI MCHEZO WAIPIGA CHELSEA 3-0 EMIRATES STADIUM

Ozil akiifungia Arsenal bao la tatu dhidi ya Chelsea




 Arsenal sasa imepanda mpaka nafasi ya tatu baada ya ushindi waliopata dhidi ya wapinzani wao Chelsea wa mabao 3-0 kwenye uwanja wa Emirates leo hii. 

Alikuwa Alex Sanchez alieanza kupeleka maumivu kwa Chelsea kwa bao lake la dakika ya 11 huku ndani ya dakika mbili mbele Theo Walcot anafunga bao la pili ndani ya dakika ya 14 ya mchezo na Mesut Ozil akikamilisha hesabu ya mabao ndani ya dakika ya 40 kabla ya kwenda mapumziko. 

Wiki hii kocha Mkuu wa timu hiyo Arsene Wenger anatimiza miaka 20 toka awe kocha wa washika bunduki hao wa London.  

No comments:

Post a Comment