Thursday, September 22, 2016

HERRERA NA RASHFORD WAMTOA MOURINHO KWENYE MATATIZO,UNITED IKISHINDA 3-1 UGENINI.

Ibrahimovic na Herrera wakimpongeza Rashford baada ya kufunga bao la 3

Baada ya mfululizo wa kupoteza mechi tatu hatimae Jose Mourinho atakuwa na tabasamu moyoni mwake baada ya timu yake ya Manchester United kuibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Northampton katika kombe la Ligi hapo jana.  


United ndio walikuwa wakwanza kufunga kupitia Michael Carrick dakika ya 17 kabla ya wenyeji kupata penati iiyofungwa na Alex Revell ambayo ilifanya United kuwa katika wakati mgumu.

Alex Revell celebrates his goal
Alex Revell akishangilia bao lake dhidi ya United
Lakini Herrera alisawazisha kabla Rashford alietokea benchi kukamilisha kalamu ya mabao kwa United na kutoka kifua mbele ugenini kwa 3-1.  
Na kwa matokeo hayo sasa United watavaana na mahasimu wao Man City katika hatua ya nne ya Kombe hilo.
  

No comments:

Post a Comment