Saturday, September 17, 2016

KILIMANJARO QUEENS KUCHEZA NUSU FAINALI NA UGANDA JUMAPILI.


Timu ya taifa ya Tanzania Bara ya wanawake Kilimanjaro Queens, inatarajia kucheza mchezo wake wa Nusu Fainali dhidi ya Uganda jumapili hii, baada ya hapo jano kumaliza bila kufungana na Ethiopia katika mechi za kundi B, katika Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati [CECAFA] mjini Jinja, Uganda. 

Matokeo hayo yanawafanya K'njaro Queens kucheza Nusu Fainali na wenyeji Uganda. Na Kenya na Ethiopia zikikutana kwenye Nusu Fainali nyingine, na jumatatu itakuwa mapumziko ya michuano hiyo kabla ya Fainali yenyewe itakayofanyika siku ya Jumanne Septemba 20 na itatanguliwa na mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu.    

Inakuwa Fainali ya kwanza CECAFA kwa wanawake ambayo itachezwa Sepetemba 20.          

No comments:

Post a Comment