Thursday, September 15, 2016

SYKORA APIGA GOLI SEKUNDE YA 12 NA KUWEKA REKODI EUROPA LEAGUE.


                               Sykola akifunga goli lake lililomuingiza kwenye historia EUROPE LEAGUE


Kiungo wa timu ya Slovan Liberec Jan Sykora alihitaji sekunde 12 tu kufunga goli liliomuingiza kwenye kitabu cha rekodi ya Europa League kama bao la mapema zaidi katika historia ya michuano hiyo Alhamisi hii dhidi ya Qarabag kwenye uwanja wa Dalga Arena kwenye mchezo wa kundi J.  

Sykora amevunja rekodi iliyowahi kuwekwa na Vitolo kwa Sevilla kwenye ushindi wa 3-1 dhidi ya Villarreal March 2015. 

Na hizi ni rekodi za magoli yaliyowahi kufungwa mapema zaidi kwenye Europa League.                          

      
Rank Player Time Year
1 Jan Sykora Slovan Liberec 9.00 2016
2 Vitolo Sevilla 13.21 2015
3 Ismael Blanco AEK Athens 15.19 2009
4 Keita Balde Ludogorets 16.88 2014
5 Juan Mata Valencia 18.18 2010
6 Sergio Aguero Manchester City 19.19 2012
7 Taison

Na kwenye Champions League goli la mapema zaidi na lililopo kwenye historia ni la Roy Maakay 2006-2007, pale mchezaji huyo wa Bayern Munich alipofunga goli ndani ya sekunde 10.12 dhidi ya Real Madrid kwenye hatua ya 16 bora.





No comments:

Post a Comment