Wednesday, October 19, 2016

DSTV YAZIDI KUWAPA RAHA WATANZANIA

Meneja Undeshaji MultChoice Tanzania, Ronald shelukindo akiongea kwenye hafla hiyo.

Hapo jana tarehe 18 Oktoba 2016, kampuni ya MultiChoice Tanzania imepunguza gharama za bidha zake ili watanzania waweze kuzimudu kuanzia Novemba mosi.

Kwa mujibu wa Meneja Muendeshaji wa MultiChoice- Tanzania, Baraka Shelukindo, hatua hiyo imechukuliwa ili kuwapunguzia gharama wateja na kwa uhondo zaidi.

Shelukindo alisema kuwa wameamua kunufaisha wateja wake kwa kufanya mapinduzi makubwa kupitia punguzo la bei na kuongeza chaneli 8 kupitia huduma yake ya DStv.

Huduma hizo mpya za punguzo la bei zitaanza rasmi kufanya kazi kuanzia tarehe Novemba mosi, ambavyo ni DStv Premium, Compact Plus, Compact, Family na Access.

DStv Premium imefanya punguzo la asilimia 16, ambapo bei mpya sasa itakuwa Sh 184,000 wakati bei ya zamani ni Sh 219,000 wakati DStv Compact Plus, imepunguzwa kwa asilimia 17 na sasa itakuwa sh 122,500 (zamani Sh 147,000) Compact ya kawaida sasa ni Sh 82,250 wakati zamani ni Sh 84,500.

Alisema sasa kifurushi cha familia, ambacho sasa kitakuwa Sh 42,900 badala ya bei ya awali ya Sh 51,000 kwa mwezi.

No comments:

Post a Comment