![]() |
| Reuben baada ya kupata nafuu. |
Mwanafunzi aliyefahamika kwa jina la Reuben Nsemoh miaka 16 katika shule ya Geogia High School alipigania maisha yake baada ya majeraha ya kichwa aliyopata katika harakati za kuokoa mpira golini kwake akiwa yeye kama golikipa, na alipokuwa chumba cha watu mahututi alizinduka na kuanza kuzungumza lugha ya Kihispania kwa ufasaha, lugha ambayo hakuwai kuizungumza hapo awali jambo lililowashangaza watu wengi.
Kinda huyoaliiambia WBS Radio Georgia kwamba huenda lugha hiyo amejifunza kutoka kwa marafiki zake na kaka zake ila anataka uwezo wake wa kuongea kiingereza hurudi.
Nsemoh alisema kwamba anataka kurudi tena uwanjani akaendelee na majukumu yake ya awali ya kipa, ingawa kocha wake amesema kwa sasa ni mapema mno kusema kwamba kinda huyo ataendelea kwenye timu hiyo.

No comments:
Post a Comment