Wednesday, October 19, 2016

LEICESTER WANG'ARA UEFA, BUFFON AKIONGEZA HESHIMA JUVENTUS.


Klabu ya soka ya Leicester City imeendeleza wimbi la ushindi katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya FC Copenhagen.
Wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani King Power, Leicester walipata bao hilo dakika tano kabla ya kwenda mapumzikoni kupitia kwa Riyad Mahrez aliyekuwa katika kiwango cha hali ya juu baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Mualgeria mwenzake Islam Slimani.

Kwa matokeo hayo Leicester wanabaki kileleni mwa kundi G wakiwa na alama 9 baada ya kushinda michezo yote mitatu ya ufnguzi wa ligi ya mabingwa Ulaya.
Timu pekee zilizowahi kushinda michezo mitatu ya ufunguzi katika michuano hiyo ni AC Milan, Paris St-Germain, Juventus na Malaga.

kwa upande wa Juventus kipa wao mkongwe Gianluigi Buffon aliibuka shujaa kwa timu hiyo baada ya kuokoa penati ya Alexandra Lacazzete na kufanya idadi ya penati zilizookolewa kufikia nane kwa msimu huu wa klabu ya mabingwa Ulaya kati ya kumi na tatu. Na katika mchezo huo Juventus walishinda 1-0.
 

Matokeo mengine ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya

Bayer 04 Leverkusen 0-0 Tottenham Hotspur F.C.
CSKA Moscow 1-1 AS Monaco FC
Real Madrid 5-1 Legia Warsaw
Sporting 1 -2 Borussia Dortmund
Club Brugge 1-2 FC Porto
Dinamo Zagreb 0- 1 Sevilla

Leo kukiwa na michezo itakayoendelea na mkubwa zaidi ule wa Barcelona na Man City utakaopigwa NouCamp mchezo unaotazamiwa kuwa na upinzani mkali.




























No comments:

Post a Comment