Thursday, October 20, 2016

SIWEZI KUBADILISHA AINA YANGU YA UCHEZAJI-GUARDIOLA


Licha ya kupoteza hapo jana dhidi ya timu yake ya zamani Barcelona, Meneja wa Manchester City Pepe Guardiola amsema kuwa hatobadili filisofia yake licha ya klabu yake kufungwa 4-0 na Barcelona katika uwanja wa Nou camp.


Lionel Messi alifunga hat-trick dhidi ya Manchester City iliokuwa na safu ya ulinzi ilio legea huku kipa Claudio Bravo akipewa kadi nyekundu kwa kushika mpira nje ya eneo hatari.hakutakuwa na mabadiliko.

''Hadi siku ya mwisho ya kazi yangu kama mkufunzi nitajaribu kucheza kwa uwezo wetu'',alisema.
Barcelona inaongoza kundi C na pointi tisa ,ikiwa mbele kwa pointi tano.

City ilikuwa nyuma kwa bao moja katika dakika za kwanza za kipindi cha pili wakati Bravo aliposhika mpira na bahati mbaya ukamuangukia Luis Suarez.

Guardiola alisema kwamba mchezo ungekuwa wazi kama wangekuwa 11, ''tumepoteza 4-0 lakini sisi ni klabu mpya, tuanhitaji kujuana, ni klabu ambayo kwa miaka 35 ilikuwa nje ya Europe.'' 

 ''Tumekuja hapa kucheza na utu mkubwa lakini siku zote ni ngumu kucheza na Barcelona wakiwa 11 kwa 10 kwenye mchezo.
 

No comments:

Post a Comment