![]() |
| Rais wa CONCACAF Victor Montagliani |
Rais wa CONCACAF Victor Montagliani amesema umefika wakati wa wao kuachana na mfumo wa zamani wa aina ya kufuzu Kombe la Dunia. Anataka kujikita zaidi kwenye kusaidia timu ndogo kwenye Shirikisho hilo.
Hali hiyo itapelekea CONCACAF kuweza kuwa na mfumo mpya wa kuweza kufuzu Kombe la Dunia 2022. Angalau itakuwa ahueni kama rais wa shirikisho hilo Montagliani atatimiza lengo lake.
Hivi karibuni alichaguliwa rais na kuiita CONCACAF ya muundo wa ''kizamani'' na alisema anatarajia kushinikiza hivyo kwamba nchi ndogo sio kuondolewa mapema. Anadhani ni muhimu kwa shirikisho kufanya kazi vizuri na kutunza wanachama wake wote, si tu kwamba kuwa na nafasi ya kufuzu nafasi ya Kombe la Dunia.
''Kuna kitu kinahitaji mabadiliko huwezi kuwa na asilimia 85 ya wanachama wako ambao wako nj'e kuangalia katika miaka miwili kabla ya Kombe la Dunia ,'' Montagliani aliiambia Associated Press,'' haina mantiki.
''Ni vizuri kwa timu hizo sita kuwepo kwenye Kombe la Dunia kwa mwaka ujao lakini vipi kuhusu hizo nyingine? Ni ngumu.''
Katika muundo wa sasa ni timu sita tu ndizo zinazobaki mpaka hatua ya mwisho na kufuzu, rais huyo amesema wanapaswa kuachana na mfumo huo aliouita wa kizamani ili kutoa kipaumbele zaidi kwa wanachama wengine.

No comments:
Post a Comment