Monday, October 10, 2016

VIWANGO VYAWATUPA NJ'E YA NNE BORA NADAL NA FEDERER.

Roger Federer and Rafael Nadal
Federer na Nadal katika moja ya mechi zao.
Waliowahi kuwa mabingwa namba moja wa mchezo wa tenisi duniani Rafael Nadal na Roger Federer kwa mara ya kwanza ndani  ya miaka 13 wametupwa nj'e ya nne bora kwenye viwango vya mchezo huo.
Mabingwa hao ambao toka 2003 hawajawai kushuka kiwango kama ilivyotokea mwaka huu, ambapo Nadal akishika namba tano na Federer akiwa namba saba, wote wawili wameshashinda mataji ya Grand Slam mara 31 katika maisha yao ya mchezo huo. 

Tatizo kwa wote likiwa majeruhi yaliyowakabili kwa kipindi cha karibuni, Federer ambaye alikuwa nj'e ya uwanja toka Wimbledon kutokana na majeraha ya goti. Huku Nadal ambaye toka Grand Slam ya 2014 alikuwa nj'e kutokana na kuathiriwa na kujiumiza mwenyewe katika miaka ya hivi karibuni.   

Huku Novak Djokovic akiendelea kuwa namba moja kwa ubora duniani kwa upande wa wanaume kwa mchezo huo, nafasi ambayo amekuwa nayo toka Julai 07, 2014.

No comments:

Post a Comment