Wednesday, October 5, 2016

XI YA CRUYFF ALIYOKUWA ANAIKUBALI MAISHANI MWAKE IMETAJWA

 


Wafusi, wadau na mashabiki wengi wa soka duniani wanasubili kwa hamu kitabu kinachoelezea maisha ya aliyekuwa mchezaji mkongwe na mwenye heshima kubwa kwenye klabu ya Barcelona na timu ya taifa ya Uholanzi marehemu Johan Cruyff's ambaye kwenye kitabu hicho ametaja kikosi chake bora cha wakati wote alichokikubali maishani mwake.

Katika kitabu hicho mkongwe huyo ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa Barca na baadaye kuwa kocha wa timu hiyo aliwataja wachezaji ambao amewaelezea kuwa walikuwa muhimu kwenye soka la Hispania, pamoja na aliye kuwa mchezaji wa Real Madrid Alfredo Di Stefano na Pep Guardiola ambaye aliwahi kuwa kocha wa Barcelona ambaye pia alifundishwa na mkongwe huyo Camp Nou 1990-1996. 
       Image result for johan cruyff images

Pia alimtaja Mholanzi mwenzake aliowahi kuwa nae timu moja huku akiwajumuisha Diego Maradona, Pelle, Garrincha, na Franz Benckebauer huku akisema safu kamili ya ushambuliaji. 

Orodha yake kamili ni-
 
Lev Yashin; Carlos Alberto, Beckenbauer, Pep Guardiola, Ruud Krol; Alfredo di Stéfano, Bobby Charlton, Garrincha; Maradona, Pelé, Piet Keizer.



No comments:

Post a Comment