Monday, October 24, 2016

ZAMALEK WASEMA NDUMBA NDIZO ZILIZOWAFANYA WASHINDWE.

Mwenyekiti wa Zamalek, Mortada Mansour.

Baada ya hapo jana kupokea kipigo kutoka kwa Sundowns katika fainali ya ligi kuu barani Afika,Mwenyekiti wa Zamalek Mortada Mansour amelaumu "uchawi na bahati mbaya" kwa kushindwa kwa timu yake mikononi mwa timu ya Afrika Kusini ya Mamelodi Sundowns.

Mwenyekiti huyo amesema kwamba "kulikuwa na nafasi nyingi kwetu sisi katika mechi zote, lakini mpira ulikataa kutingisha nyavu" Mansour aliongeza, baada ya kushindwa mabao 3-1 kwa jumla ya mabao.

''Hivi inawezekana kweli hukose nafasi 18 mbele ya goli? mambo hayakuwa sawa kweli kulikuwa na nguvu za giza na uchawi.'' Aliongezea  Mwenyekiti huyo. 
 
Moamen Soliman kocha Mkuu wa Zamalek.
Pia aliunga mkono kwa kocha Moamen Soliman kusalia katika nafasi yake licha ya kupoteza.

"Tuna wakufunzi wazuri na sitawafuta kazi," amesema Mansour, mbaye aliwatumia wakufunzi sita mwaka huu.
"Kocha Moamen atasalia kama mkufunzi mkuu wa Zamalek, hadi mwisho wa msimu huu."

Mabingwa hao wapya watacheza  Kombe la Dunia la klabu nchini Japan.
Mafanikio ya Sundowns kuwa klabu yenye ushindani yamekuja miaka 21 baada ya klabu ya Orlando Pirates kuwa timu ya kwanza ya South Africa kushinda taji hilo.

No comments:

Post a Comment