Wednesday, November 9, 2016

VPL MZUNGUKO WA KWANZA KUFIKIA TAMATI KESHO.


Mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara unafikia tamati leo na kesho. Simba leo inashuka dimbani kwenye Uwanja wa Sokoine Mkoani Mbeya kucheza Prisons huku Yanga kesho akicheza na Ruvu Shooting.
Sababu ya kuvuta nyuma michezo hiyo ni kutoa nafasi ya maandalizi ya kambi ya timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inayotarajiwa kusafiri Ijumaa wiki hii kwenda Harare Zimbabwe kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa unaotarajiwa kufanyika Novemba 13, mwaka huu
Simba inaongoza ligi kwa pointi 35 mbele ya pointi tano dhidi ya Yanga. Simba ambayo iliteleza wiki iliyopita kwa kukubali kipigo kutoka kwa African Lyon cha bao 1-0  na kutibua rekodi yao ya kutopoteza mechi toka msimu huu wa ligi uanze. kwa miaka minne mfululizo mnyama hajashiriki michuano ya Kimataifa na mwaka huu kuonyesha kurudisha hadhi yao kwa kujihakikishia kuchukua ubingwa kwa mara ya 19.


Wafungaji wanaoongoza kwenye raundi ya kwanza.
Kwa upande wa wafungaji bora mpaka sasa Shiza Kichuya wa Simba anazidi kuwakimbiza ikiwa na mabao tisa hadi sasa, akifuatiwa kwa karibu na Amis Tambwe wa Yanga mwenye mabao saba akikabana koo na Rashid Mandawa wa Mtibwa Sugar naye ana mabao saba.

Simon Msuva wa Yanga mabao sita huku wenye mabao matano wakifungasha wachezaji sita ambao ni Omary Mponda, Riffat Khamis (Ndanda), Abdulrahaman Musa (Ruvu Shooting), Obrey Chirwa, Donald Ngoma (Yanga) na John Bocco (Azam).

No comments:

Post a Comment